Ujumbe kutoka Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu watembelea na kufanya mazungumzo na Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Addis Ababa tarehe     15 Septemba, 2021.  Ujumbe wa Mahakama uliongozwa na Rais wa Mahakama ya Afrika, Mhe. Jaji Iman D. Aboud

Mazungumzo yalijikita katika kuimarisha uhusiano kati Mahakama na Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika, nafasi ya Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu katika kufanikisha utekelezaji wa malengo ya Umoja wa Afrika na namna ya kushughulikia changamoto zinazoikabili Mahakama hiyo.  

  • Mhe. Elizabeth Rwitunga, Kaimu Balozi (wa nne kutoka kulia) na Rais wa Mahakama ya Afrika, Mhe. Jaji Iman D. Aboud (wa tano kutoka kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wengine wa Ubalozi na Mahakama.Mhe. Elizabeth Rwitunga, Kaimu Balozi (wa nne kutoka kulia) na Rais wa Mahakama ya Afrika, Mhe. Jaji Iman D. Aboud (wa tano kutoka kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wengine wa Ubalozi na Mahakama.